Wednesday 30 December 2009

KIKWETE ANGOJEA HISANI YA MAKADA

Wakati miezi takribani tisa imebaki kabla ya uchaguzi mkuu,jahazi la mkuu wa nchi inaonekana kupoteza nguvu katika chama na hata makundi ya kijammii.

Kikwete anakabiliwa na upinzani mkubwa sana, unaohatarisha nafasi yake kushinda kuwa mgombea wa chama chake, hii inatokana na mahusiano yanayojengwa na katibu mkuu Makamba, kutothamini mawazo ya wakongwe kama akina joseph Warioba ,Dk salim Ahmed salimu,

kitendo kinachoendelea kujenga makundi,ambayo inadhaniwa uwenda yakamuunga mkono,FREDRIC SUMAYE pindi atapotangaza azma yake ya kugombea urais.

Makada mashuhuri wamesikika wakisema, chama hakiwezi kuendeshwa kwa vitisho na matusi, bali hoja na kufuata misingi na hitikadi ya chama.
Imefika wakati viongozi wa chama wanadhubutu kuwahita wanachama wengine wehu, watu walioshika nyadhifa mbalimbali. na bado wengine wakiwa wanamajukumu mbalimbali ya kichama.

Kwa upande wa wananchi wa kawaida wanakiona kitendo cha rais kuwa kimya huku rasilimali za taifa zikiibiwa kwa kisingizio cha mikataba ya kimataifa ni uzembe unaoligharimu taifa.

Tazama misamaha ya kodi pamoja wanayopewa wageni katika nchi yetu ni mikubwa kuliko katika nchi yeyote.
Cha kusikitisha ni unaposikia waziri anasema makampuni hayajarudisha mitaji waliowekeza.

Huu ni ukosefu wa mtazamo ,kusubiri wawekezaji wapate faida, kwani mbona mwananchi wa kawaida anapowekeza katika biashara mfano daladala, anaanza kulipa kodi moja kwa moja na hangoji mpaka kurudisha mtaji wake.

Kutokana na mapungufu yaliyojitokeza katika utawala wa awamu ya nne. Ambayo yameiingiza nchi katika udini, ukabila na kambi za kisiasa.

Imesababisha kujiwekea watika mgumu wa kurudi kipindi kingine kwani nani ambaye hafahamu nguvu za kambi ya mwandosya ,ya akina salim ahmed salimu na fredric sumaye pindi zitapojiunga.

je kikwete anaweza kukabiliana nazo au atamtumia makamba kujibu hoja kwa matusi.

Ni vema rais kikwete, akaonyesha mfano bora katika taifa letu, kwa kutogombea tena, kwani atakuwa amejijengea heshima kubwa ya kutong"ang"ania madaraka.

kwa kadri ninavyomfahamu kikwete hashindwi kutogombea tena, lakini shinikizo kubwa linatoka katika wafuasi wake ambao walichangia kampeni kwani wengi wao hawajachota faida za kutosha.

Bila ya mabadiliko CCM inaifuata historia KANU na ZANU PF,kwani nani aliyeota ndoto kwamba KANU kitatoweka katika siasa za Kenya , au ZANU PF katika siasa za Zimbabwe?

Serikali ya CCM imepoteza vipaombele, imebaki kucheza ngoma ya maisha bora kwa kila mtanzania, ari mpya kasi mpya na kilimo kwanza .

Cha msingi cha kujiuliza ni nini kitatufanya kuendelea kumuunga mkono rais wa kambi mojawapo ya CCM, kwani wote tunafahamu CCM ilitokana na muungano wa TANU na ASP lakini kadri siku zilivyoenda nguvu ya CCM ikatawaliwa na waliokuwa wanachama wa TANU.

Lakini mgogoro wa sasa hautokani na wanachama wa ASP na TANU. si mvutano kati ya wazanzibar na wabara ndani ya chama kwani wazanzibari walishasalimu amri na kuachia nguvu za chama ndani ya wabara.

Mgogoro wa sasa unatokana na watawala wa sasa kutotaka kusikiliza ushauri wowote toka kwa kambi zilizoshindwa 2005, hivyo basi kuzifanya kambi hizo kama vikundi vya wahaini.

Kwa upande wetu wananchi tunafurahi kwani makundi ndani ya CCM yamefanya tufahamu mengi kuhusu madhara gani ya kununua madaraka.kambi ndani ya vyama zinamadhara gani?

Kugawanyika ndani ya CCM ni funzo kubwa kwa vyama chipukizi kama UDP, NCCR
CHADEMA n.k kwamba lazima waunde umoja na kutoa elimu kwa wanachama ya ni jinsi gani ya kuendesha siasa ndani na nje ya chama.

Mwalimu NYERERE hakukosea kuanzisha chuo cha mafunzo kivukoni,kwani kilichangia kuimarisha siasa za chama ndani na nje na kujenga mifumo ya uongozi katika sekta ya siasa.

lazima wanachama kama Makamba na Tambwe hiza muhamiaji toka CUF watambue kejeli si sera za chama kwani zinaongeza mgawanyiko.

Siasa na unajimu ni vitu tofauti huwezi ukaongoza nchi kwa kufuata wapigaramli na wanajimu kwani yuko wapi Mobutu seseseko na kundi lake la wapunga pepo, wapunga pepo walimtabilia kwamba angeshinda vita zidi ya Banyamulenge matokeo yake ni kushindwa kwa kishindo.

Tamko la ikulu kuhusu wapigaramli limetushitua kidogo kuhusu je ikulu imeamua kuanza siasa za maruani au kwa nini watoe ufafanuzi kuhusu tamko hilo, kuna mawazo mangapi yamepingwa au kutotolewa ufafanuzi.

Kushindwa kwa siasa za sera,kunapelekea kubadilika kwa siasa toka wito kuwa uhadui na kuhatarisha amani na mshikamano wa nchi yetu.

Kikubwa tunachokiona ni kukoma kwa sera zilizopo. Ni lazima zibuniwe zitazoendana na wakati, kwani tatizo si kwenye vyama vya siasa tu bali ata katiba nayo ni tatizo ukisoma katiba kuna vifungu vinavyopingana na vingine vikikandamiza jamii fulani.

mgawanyiko ndani ya CCM umemuweka rais katika wakati mgumu na ikisadikika ndio unaochangia kuzorota kwa afya yake na kusababisha kuanguka mara kwa mara.

nakama hii ndio sababu ya kuanguka kwake, sisi wapitanjia tunapatwa na hofu kubwa. kama afya ya kiongozi mkubwa wa nchi yetu, kwani si lazima uwe daktari ili utambue kwamba wagonjwa wanamahamuzi gani? je nchi yetu inamfumo gani wa kuzuia mahamuzi mabaya yanayoweza kutolewa na rais wa jamhuri ya Tanzania.

Mgongano ndani ya CCM unasababisha jamii itambue siasa zina faida kiasi gani na malengo ya wanasiasa ni yapi? kwani kama siasa isingekuwa na faida vikumbo kati ya wagombea ubunge na urais vingetoka wapi? na siasa chafu ndizo zimepelekea kumweka rais katika wakati mgumu , ata kupelekea kuiweka hatma ya rais mikonomi na hisani ya makada wa chama hicho.

hii ni hatari kubwa kwani inaweza kupelekea rais kufikiria kutumia madaraka yake ndani ya serikali kuzima uhasi ndani ya chama chake.

Taifa na vyama vya siasa lazima viangalie maslai ya taifa kwa kuboresha mifumo yake ya kiutendaji kwa mfano haikuwa sahihi kwa makamba kutumia kauli ya chama kwamba kitamuunga mkono 2010 bali alitakiwa aseme yeye kama yeye atakuwa katika kambi ya Kikwete kwani wanachama wote wanahaki ya kuomba nafasi stahili ndani ya chama chao.

Mbona wabunge waliotawala kipindi kimoja wanajitokeza wapya kuwapinga? au Cheo cha katibu mkuu wa Chama ni cha usemaji wa rais.

Makamba ana mengi ya kujifunza lakini hili la matusi na kejeli limesababisha kidonda kikubwa ndani ya chama chake na ata mustakabali wa rais.

Natoa wito kwa wanachama wa CCM wataojitokeza kupingana na rais 2010 wajitokeze si tu kwasababu wana chuki na rais bali wana uwezo wa kuongoza taifa la Tanzania na ni haki yao ya msingi.

siasa ndani ya CCM lazima iwe kwa misingi ya sera na si makundi na chuki, kwani kuendeleza chuki kutapelekea uhasama na kudunisha maendeleo ya jamii ya Tanzania.

Ushauri wangu kwa kikwete kama anaona nayeye pia anaweza kuongoza kipindi cha pili agombee kwa hiari yake na si kushinikizwa na wapambe kwani kila mtu atapima kina cha maji kabla ya kujitosa.

Mungu ibariki tanzania
Godwin chacha 0718122081
www.godwinchacha.blogspot.com

Tuesday 1 December 2009

NINI KIFANYIKE TANZANIA

NINI KIFANYIKE TANZANIA
Tanzania ni nchi iliyojengwa katika msingi wa ujamaa na kujitegemea, chini ya utawala wake, hayati baba wa taifa mwalimu julius k.nyerere.Ujamaa ni mfumo uliowapa fulsa sawa jamii yote ya tanzania upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii kama elimu afya nahata nafasi ya uongozi jamii yote bila ya kujali wametota katika jamii gani.Baba wa taifa aliweka misingi ya uongozi wazi, na hata tukawa na Azimio la Arusha, lililotamka wazi, nini kifanyike kwa viongozi na watu kwa ujumla.

Misingi hii ilisaidia kuwabana watu wenye uchu na ufujaji wa mali na rasilimali za taifa, kushindwa kufanya hivyo.Hatusemi kwamba chini ya utawala wa baba wa taifa hakukuwa na urasimu, kwani wote tunafahamu wakati mwingine, ugawaji wa bidhaa kama sukari na unga wakati mwangineulifanywa kwa urasimu(uranguzi) na watumishi wa serikali yake .
Lakini kikubwa tunachojivunia ni pindi tatizo lilipojitokeza hakusita kuchukua hatua, yeye kama kiongozi.
watu waliachishwa kazi na wengine ata kuchapwa viboko.

lakini misingiya taifa ilianza kubomoka katika utawala wa raisi Mwinyi,ambapo kulikuja kuibuka Azimio la Zanzibar.
Azimio la Zanzibar, Liliruhusu viongozi kuanza kujilimbikizia mali, na hata wachache kumilikishwa uchumi wa taifa, hapo ndipo pengo kubwa kati ya walionacho na wasionacho lilipoibuka.
Hatupingi jamii kutofautiana kwa kipato, lakini watofautiane kwa haki na si wengine kwa kuhujumu wenzao.

Ubinafsi ulianza kuota mizizi na pindi serikali ya hawamu ya tatu ya bwana Mkapa wakahitimisha ugawaji wa mali za umma kwa wachache.kukatokea na uhibukaji wa watu wenye uchu wa mali, sijui walitokea wapi. Kwani hata wengine ambao si watanzania wa kuzaliwa, waliona kuna fursa wakakimbia kuchukua uraia wa Tanzania, na kuanza kushiriki katika wizi wa mali za umma.

Cha kujivunia katika utawala wa tatu nchi haikutikisika na mshikamano bado haukuvuvinjika na wananchi hawakukata tamaa.
Katika awamu ya nne ikisadikika iliingia madarakani kwa michango mingi kutoka kwa watu binafsi.

Awamu ya nne Iliwapa wananchi tumaini ya kurejea kwa maisha bora, na upatikanaji wa huduma muhimu za jamii.Ilianza kwa kishindo na kila mtu akadhani ni wakati wa mabadiliko makubwa ya kiutawala na ya kuwa Taifa linaelekea ambapo,jamii yote itanufaika na rasilimali za Taifa lao.

OH sipende hata kuamini mambo yanayotokea katika Taifa letu,mbali na
kujilimbikizia mali , wachache wezi wamekuwa na sauti ya kuwatukana watu wanaotetea haki ya taifa lao.
viongozi wakuu wakitetea wizi uku utawala unaona.JE ndio sera za awamu hii?.Taifa linateteme na mbaya zaidi unasikia watumishi wakubwa katika uongozi wakisema wazi, kijana usihoji wizi, mbona siku yeyote taifa linaweza kuingia katika eneo ambalo historia ya amani katika nchi yetu ikatoweka.
Dini zimetengana,jamii imeanza kuzomeana kati ya wezi na wapinga wizi,Siasa imegeuka biashara,uporaji mkubwa wa rasilimali,uroo wa madaraka,
mgawanyiko wa matabaka, wazee na vijana, maskini na matajiri, udini,ukabila,kushindwa kuwa na falsafa yeyote inayojulikana ambayo taifa inaifuata,

Tunajiuliza nini mustakabali wa nchi,ninani atayeweza kurudisha mambo katika mstari?.
Si kugawanyika kwa viongozi bali tazama hata sekta ya habari, mafisadi wameanzisha vyombo vya habari. wakijitangaza na kujigamba hakuna mtu anayeweza kuwagusa,inamaana wao wananguvu kuliko serikali au wao ndio wamiliki wa serikali?,

Kwa upande wangu mimi ninaona suruhisho lipo katika njia mbili,
wananchi waitishe makongamano mbalimbali juu ya nini wanahitaj kifanyike, nini kusifanyike. Hatua gani wanahitaji zichukuliwe, au zisichukuliwe, na kama zisipochukuliwa ni nini cha kufanya?.

Pia misingi ya viongozi tunataka iweje? mfumo wa uongozi,kuanzia wa kisiasa mpaka kiutendeji,kwani madaraka ya raisi yawekwe wazi katika maamuzi, na uteuzina. Kama wakiona hakuna maamuzi ya msingi anayofanya nini kifanyike.je mbali na nguvu ya bunge kuisimamia serikali je wananchi wananafasi gani?.

Kwa upande wa pili ni kwa serikali kutangaza wazi kupitia, kwa raisi na watendaji wakuu ,nini msimamo wa serikali. Je nchi ihachwe iende kadri inavyotaka, au kuna mahamuzi magumu yanahitajika kuchukuliwa?. Uwajibikaji gani unahitajika. wapi kuna tatizo, wapi wanahitaji msaada?,nani wanasita kumchukulia hatua? kwanini wanasita kuchukua hatua?nini walikopa,kwa nani na wanahitajika kulipa nini?.

Mbali na misingi ya uongozi ni vipaombele gani vifuatwe kwani, kila bajeti tunasikia ina kipaombele chake,kama ni kilimo basi razima maamuzi yachukuliwe,ionekane wazi mikakati ya taifa, si mikakati ya kampeni.
Kama ni viwanda ni viwanda gani tunavitilia mkazo, mfano tunaweza kujitosa katika viwanda vya kilimo, na uboreshaji wa madini na vito vyetu.serikali na jamii inaweza kuendelea kwa namna hiyo.

Baba wa taifa aliwahi kutoa wazo la nchi kuendelea inahitaji, watu ardhi,siasa safi na uongozi bora,je tanzania ya sasa tunataka kupunguza vitu viwili, kutoka katika orodha yake? yani siasa safi na uongozi bora?.

Nahisi taifa ni wakati wake kujipima na kufanya marekemisho, hatua za msingi ili liweze kupata maendeleo, tunaipenda tanzania na daima hatupo tayari kuona inaelekea pabaya,tunaomba wananchi na viongozi kwa ujumla, kuchukua hatua, za kuboresha na kufanya marekebisha yanayoitajika. ili kuondoa manung"uniko,kuleta haki,huwajibikaji na kulinda rasilimali za taifa letu.
MUNGU IBARIKI TANZANIA
GODWIN CHACHA
0718122081
www.godwinchacha.blogspot.com

Monday 23 November 2009

TANZANIA IMEJISAHAU

tanzania ni miongoni ya mataifa yenye utulivu utulivu huu usiwafanye watawala kufanya ndio misingi ya kukandamiza jamii fulani tumeshuhudia polisi wakitwa wazembe na waheshimiwa sipingi kwani hata walimu na wanajeshi nao utendaji kazi wao umeshushwa na upungufu wa maslahi duni na ukosefu wa vitendea kazi watawala wameamua kuwaingiza katika mtego utaowatofautisha na wananchi kwa kuwahusisha na ufisadi wa meremeta watawala wanatumia misingi ya nidhamu ya jeshi kutowajibika kujibu hoja yeyote iliyotolewa na mkubwa wako, napenda kusisitiza kwa watawala wasijaribu kutibua misingi mizuri ya jeshi na kulitwisha mzigo wa ufisadi, ningependa kuwafahamisha ya kuwa mzigo wa ufisadi ni vema wachague ni fisadi gani atayeubeba na si jeshi kwani utakua ni uonevu usiostahiri na utaoleta madhara makubwa kwa watawala wenyewe ni nani asiyefahamu kutoa kafara wapiganaji wetu kuna madhara gani? sipendi kuona watanzania tunapoteza misingi ya amani na utulivu ila nasita kuona ni wapi jahazi la tanzania linaelekea , vijana wapo tayari kulikomboa taifa lao kutoka katika dimbwi la umasikini hata kwa dhana duni ila watawala wawahakishie sera bora tunaweza kushiriki katika kilimo lakini taifa ni lazima litunze ardhi kwani sasa taifa linabinafsisha kwa wageni ningependa tusiliingize jeshi katika ufisadi ila ikibidi lishirikishwe kwenye uzalishaji na miradi kama nyumbu inaweza kuleta tija na heshima kwa jeshi letu sishangai kuona viongozi wakijisahau kwani ni kawaida kwa binadamu wasio na uwezo wa kukumbuka ni wapi walipotoka ni nani asiyejua ni askari wangapi wanalala njaa na kushindwa kusomesha watoto wao vyuo vikuu kutokana na sera za watawala wanaojari maslai yao na kutaka kujinufahisha kupitia wanyonge,natambua tanzania ni tajiri kwani mimi kama mwanachuo ninayesomea account and finance natambua nini kinaendelea, kikubwa kinachonisikitisha ni kitendo cha watawala kutaka kuliunganisha jeshi na wakoloni sijui wamelala na kusahau wanakata tawi waliokalia kwani ni nani atayemtoa mkoloni wanayempa ardhi yetu kutokana na ukuhadi wa viongozi wetu tazama watawala wanavyotumiwa kuteketeza maisha ya watanzania north mara (NYAMONGO) je inahitaji elimu ya chuo kutambua taifa lipo katika ukoloni mamboleo na ni upungufu wa afikiri unaosababisha umasikini wetu na kutumiwa kama mabwege na wakoloni na sasa mkoloni anasababisha kitendo cha kulipotezea imani jeshi letu ili iwe raisi kuja tena kwa kadri ninavyowafahamu watu wa kanda ya ziwa nachelea kusema serikari inaliingiza jeshi la polisi katika mgogoro usio na tija jeshi la polisi na wananchi nafahamu ya kuwa watawala wameamua kutumia jeshi vibaya kwa malengo ya kisiasa ili kuvunja sakata la ufisadi na kuendeleza ukuhadi wa wakoloni kama hawatambui ni kosa linaloweza kusababisha mabadiliko ya historia ya nchi na wao wasipate watu wa kuwatawala kwani ni nani mwenye furaha huko somalia..? kama si magaidi pekee najiuliza watawala wetu wanataka kuwa magaidi ..? wiishi kama somalia au wanapenda wawe kama MOBUTU SESESEKO....? ni kitu cha kushangaza kwa watawala wetu kutopenda kuwatumia wataalamu wetu sasa imefika wakati wanafikiri wanastahiri kujiheshimu wao tu na kutupia mzigo wa lawama kwa kila wanayemuona napenda kusisitiza ya kuwa wanajeshi si walimu kwani watawala wamewakandamiza kwa kipindi kirefu bila ya wao kujinasuo na kuongozwa na vibaraka wanaouza haki za walimu kwa SUZUKI NA RAV 4 , naipenda tanzania na nisingependa 2020 niwe mkimbizi katika ardhi ya wazungu kama wasomi wetu wwalivyozoea kudhani ya kuwa ulaya ndio kipimo cha mafanikio yao, najiuliza je watawala wanajaribu kuamsha mawe ili wao wanufaike au wawe wakibizi katika ardhi za wanaowafanya makuhadi wao na kutorosha rasilimali za taifa lao ,nisingependa kuelezea kwa undani zaidi kwani hata baba yangu aliwai kusema "WATAWALA NI JAMII YA WATU WASIO NA UCHUNGU NA RASILIMALI ZA NCHI ZAO NA NI WATU WASIOTESEKA NA VITA NA UMASIKINI WA TAIFA" nawatakia watanzania mafanikio na ushindi katika maisha ya kila siku na kushauri watawala wasiangamize kizazi kisicho na hatia MUNGU IBARIKI TANZANIA
MUNGU IBARIKI AFRIKA
GODWINI CHACHA
0718122081

Sunday 22 November 2009

BODI YA MIKOPO NA UNYANG"ANYI

GODWIN CHACHA Says:




November 12, 2009 at 11:28 am

BODI YA MIKOPO YA ELIMU YA JUU INAPOGEUKA
KIKUNDI CHA WAHUNI NA WANYANG”ANYI
Ni miaka sasa imepita toka taifa lifikilie ni jinsi gani ya kuanzisha mfumo utaowawezeza watanzania wanaotakiwa kuendelea na masomo ya elimu ya juu kupata mikopo yakuwawezesha kujilipia karo na matumizi madogo ya kila siku kama chakula nk, kutokana na sheria ya uanzishwaji Taifa lilitoa ahadi mbali mbali kuwa hakuna mtanzania atayeshindwa kusoma kwa ajili ya kukosa mkopo,lakini kama taifa likateuwa watendaji wataohusika na utoaji wa mikopo wakiwa chini ya kitengo kilichojulikana kama bodi ya mikopo ya elimu ya juu.lakini pindi kikundi hiki kilipoanza kazi kikageuza wanafunzi wanaoomba mkopo kama ni wafungwa na wao ni chombo cha kuwakomesha na kuwashikisha adabu kwa kuwachelewesha na kuwanyima mikopo maskini na kuwapa matajiri na ata wafanyabiashara wasio wanachuo mikopo na kuwatesa ipasavyo wananchi wa ngazi ya chini kwani kama bodi hii inatambua mwanachuo anatoka katika familia maskini iweje ikapita hadi miezi minne toka chuo kifunguliwe bila ya kumpatia fedha ya chakula je mtu huyu anaweza kuishi vip? na pia je inawezekanaje kwa mwanachuo kuenda katika mafunzo yake ya vitendo bila ya kumpatia pesa na badala yake watumishi hawa wanaziweka pesa zake kwenye mabenki ili wale riba, si hivyo tu bali ukisoma katika tarifa yao utaona wanawapa fedha kidogo za nauli kuliko wanazoandika na kujinufaisha,ona vijana wadogo wa taasisi hii wanaolipwa mishahara midogo kadri ya laki nne wanvyojenga maghorofa mbezi beach na masaki je huu ndio mshahara wao unavyotumika hau ni wapi wanapata pesa hizi? je kumuandikia mtu pesa nyingi za nauli na kumpa kidogo sio ufisadi? je taifa linatambua ya kuwa watu waliopewa dhamana ya kuwaudumia wasomi wanawageuza watumwa na wafungwa, napenda kutoa wito wangu kwa mfano mtu anayepewa jukumu hili kwanza awe ni mzalendo, awe na uzoefu kwani hapa si mahali pa kujifunza kazi kwenye elimu ya juu, na nashindwa kutambua ya kuwa je bodi hii inachombo chochote kinachoisimamia kwani kina uhuru mkubwa amboo unauzidi hata wa mahakama, napenda kuwafahamisha ya kuwa mimi sisemi kwa kubahatisha kwani hata leo hii wapo wanachuo wa mzumbe wlioanza mafunzo kwa vitenda oktoba 12 mpaka leo ni zaidi ya mwezi lakini pesa zao zimekaliwa na watumishi hawa wakizizalishia hili wapate riba ndio waje kuwapa je watu hawa wanajua jinsi wanachuo awa wanavyoteseka au ni namna ya mfumo wao wa kuwaadabisha kama wafungwa wao wa kielimu? mbaya zaidi wazazi na wananchi katika taifa hili kuwa kimya kwa jambo hili huu ni upuuzi kutuletea kilimo kwanza huku ukiwaacha watu wakiua elimu ya juu, hakuna taifa litaloendelea kwa kutesa wasomi wake,na kama ikitokea sisi ndio tutakuwa wakwanza kwani tumebaki kuwa tifa linalojivunia kwa kujigamba kuwa sii ndio taifa la kwanza kwa kubuni mambo, wako wapi usalama wa taifa kwani hawaoni wenzao CIA wanvyolinda maslahi ya marekani kwani ingewapasa hata kuua watu wachache hili taifa liendelee, au na usalama wa tifa wanahitaji mwekezaji? au menejimenti mpya, nisingependa kuongelea PCCB WALA POLISIkwani kila mtu anajua utendaji wao, naomba taifa lifikie mahali liwashitaki na kuwapandisha kizimbani watumishi wa bodi hii na ikibidi wafilisiwe mahekalu yao

Napenda kuwaeleza ya kuwa hipo siku watawajibika kwa wanayoyafanya sasa hata wakiwa kaburini tutafunga pingu juu ya makaburi yao ili umma utambue ujuma yao,

napenda kuwajulisha elimu ni bahari na wasizani kuna namna ya kuhuma watazozificha daima

MUNGU IBARIKI TANZANIA

MUNGU WABARIKI WANACHUO

MUNGU WALAANI WATUMISHI WA BODI



GODWIN CHACHA

MZUMBE UNIVERSITY

0718122081

TANZANIA NI SHAMBA LA BIBI

GODWIN CHACHA Says:




TANZANIA NI SHAMBA LA BIBI

kama tunavyofahamu mbali na kuwa na rasilimali za kutosha na idadi kubwa ya watu wasio na elimu bado ikisadikiwa ni taifa maskini kabisa duniani na taifa lisilonufaika na rasilimali zake kama madini na idadi ya watu ambao hawafahamu ni jinsi gani ya kunufaika na kutumia mianya kujiwezesha kiuchumi na kutumiwa kama vibaraka katika kujiibia mali za taifa lao na kutotimiza wajibu wao ikiwemo kuwawezesha wageni kukwepa kodi na pia kuwa na WABUNGE wasio na uwezo wa kulisimamia taifa lao mimi G.JUSTIN mwanabiashara wa chuo kikuu cha mzumbe ningependa kuto maoni yangu kwa raisi JAKAYA KIKWETE kwamba kutokana na mwenendo wa taifa letu ni bora achague moja kuwawajibisha watendaji wazembe kwa mfano sioni kazi ya baraza la mawaziri kwani limeshindwa wajibu na hivyo basi ni wakati wa kurekebisha katiba hili kuwawezesha watu wasio wabunge kuwa mawaziri kwani kama wabunge wameshindwa kazi yao je wakiongezewa na uwaziri wataweza ? si hivyo tu MAKAMISHNA KODI TRA ni vema wakawajibishwa kwani kutokana na ufahamu wangu na rasilimali zetu tulitakiwa tukusanye angarau TRION 5 kwa mwaka sasa kutokana na kutowajibika tunaambiwa mgodi wa WILIAMSON DIAMOND ulikuwa unajiendesha kwa hasara jamani ebu fanyeni uchunguzi mtagungua kitu ndani ya mgodi huo nasikitika kwa umaskini wetu watanzania lakini nashindwa kutambua ni nini maamuzi ya watoto wetu kwani inaonekana kizazi cha kati kimepoteza uelekeo je kizazi kipya kinachoonekana kuja na mawazo mbadara kitaweza kuokoa jahazi kabla lijazama

WAANDISHI WA HABARI

tatizo la waandishi wa habari ni kutokuwa na ujasiri wa kuandika mambo yanayoliangamiza taifa la tanzania na kuacha viongozi wafanye wanavyotaka kitu ambacho kitakuja kuleta matatizo ktk kizazi kijacho na mapambano ya wenyewe kwa wenyewe tazama kama bwana kubenea na zitto kabwe walivyo punguza misimamo katika kutetea na kueleza jinsi serikali inavyoendesha mambo yake kivificha ninachajiuliza mimi ni watu na jamii hasa wanahabari wanovyoweza kunyamaza huku taifa likishughulikia taratibu mambo kama EPA RICHMOND BOT ZOMBE BUZWAGI DOWANS IPTL WALIMU UHURU WA HABARI ningependa kutoa changamoto kwa wazalendo kama MWAKYEMBE ,ANA KILANGO,DR SLAA,OLE SENDEKA, JAKAYA,MAGUFULI,na wengineo wasimame imara kutetea wanyonge na bwana zitto rudi katika kasi yako pia KUBENEA ongeza juhudi na mapambano

MUNGU IBARIKI TANZANIA

TANZANIA INAPOELEKEA

GODWIN CHACHA Says:




May 22, 2009 at 11:59 am

kama sisi wenyewe kwa wenyewe hatusaidiani je jini gani atasimamia haki na wajibu wa viongozi wetu? kama ilivyo kawaida yetu waTZ muda mwingi tunautumia kwa kulalamika badala ya kufanya kazi na kutetea haki zetu wananchi hawafahamu kuwa hospitali elimu ni haki ya msingi vikifuatiwa na barabara na maisha bora na watambue wana haki ya kuiwajibisha serikali kutokana na uzembe na ukosefu wa maendeleo na vifo visivyo vinavyotokana na afya duni je ni kesho au leo wataanza kuoji?au wanangoja watoto wetu waje kuoji?kama nikipata nafasi na fedha kama mafisadi nitatumia muda wangu kuwaelimisha kupitia gazeti langu sio kubaki na manung’uniko ya sisi waarabu tunaonewa .je wananchi wanaweza kutambua madini sio ya viongozi bali ni yao? je wananchi wanatambua njaa si haki yao? je kufa kwa mabomu mbagala si uzembe wao? je ajila si hisani?ukuhadi una mwisho? naogopa siku wananchi watapojua aya watadai walivyoibiwa? au watapigana na waliowaibia? kutokana na upeo wangu sitambui ni janga gani linakuja lanini nahisi tanzania inaelekea pabaya.je malaika gani wataiokoa kwani mapadri na masheha wanaelemewa.kama nikifika mwaka 2020 nitakuwa nimeshuhudia ninayofikiri. je baada ya mwakyembe kuwatetea wananchi atafuata nani? je zitto nae ataanza kama zamani? je slaa ataendelea na ushujaa? na je kikwete atakuwa raisi wa kwanza kutawala kipindi kimoja? nafikiri katika maswali yangu nahitaji miaka 10 kujiuliza maswali lakini tanzania pasipo na mabunge mawili ni bure.je baada ya sitta ni spika yupi? je sitta atakua raisi? kama ningeambiwa kuchagua kazi ningekuwa mwalimu kwani kuonewa nisingeogopa.yote haya najiuliza ni nani na lini tanzania iliuzwa? nani ameinunua? je hatatufukuza katika ardhi yake? je tutaenda wapi kama tukifukuzwa. enyi wazalengo badilisheni mfumo wa mapambano sifa binafsi haziwezi kulikomboa taifa maskini lenye rasilimali nyingi.je watanzania ni vivutio vya utalii na kama tukiendelea watalii hawata kuja kutuangalia?je nasi tujute kuzaliwa tanzania

MUNGU IBARIKI TANZANIA
GODWIN WA MZUMBE
0718122081